×

Jubilee Insurance Yaja Kidigitali, Wadukuzi wa Mitandao Kunaswa

 

Meneja Maendeleo wa huduma za bima, Hussein Nassoro akizungumza jambo wakati wa hafla hiyo.

Kampumi za bima nchini zimetakiwa kuongeza Kasi ya utoaji wa elimu ya masuala ya bima kwa wananchi kabla ya kuwauzia bima hizo ili kuondokana na malalamiko yanayosabishwa na uelewa mdogo wa wanachama wao juu ya huduma na malipo yanayotakiwa kugharamia huduma husika.

Mkurugenzi Mtendaji wa Jubilee Insurance, Dipankar Acharya akizungumza jambo katika hafla hiyo.

 

Wito huo umetolewa na  Mkurugenzi wa Masoko, Mipango na Utafiti kutoka TIRA, Zacharia Muyengi wakati akizindua huduma mpya ya bima inayohusika na majanga ya udukuzi iliyoanzishwa na Kampumi ya Jubilee Insuraynce kukabiliana na wizi na uhalifu wa mitandao unaoendelea kushika Kasi katika maneo mbalimbali nchini na duniani kote.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo, ambaye ni Mkurugenzi wa Masoko, Mipango na Utafiti kutoka TIRA, Zacharia Muyengi (kulia) akikata utepe kuzindua huduma hiyo.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa program za bima wa Kampumi hiyo amesema bima hiyo Ni bidhaa mpya anayolenga kulinda nyaraka na taarifa za makampuni zinazohifadhiwa kupitia mfumo wa mitandao mbalimbali Kama Google, Yahoo Gmail na mengineo

Leave a Comment