
Kocha wa Al Ahly 🇪🇬 Pitso Mosimane amkingia kifua nyota huyo aliyeng’ara Tanzania 🇹🇿 kwa kiwango bora. Kwenye mkutano na wanahabari baada ya mchezo Al Ahly 3 – 2 Al Ghazl, Pitso alishindwa kujizuia na kupandwa na hasira alipoulizwa swali na mwandishi wa habari kuhusu kiwango cha Luis.
Mwandishi alitaka kujua kwa nini hamchezeshi kijana mdogo (Mzawa) ambaye ana kiwango bora zaidi kuliko Luis?
“Kwa hiyo unataka Luis asicheze? Kwa nini asicheze, mbona Wachezaji wengine hujauliza, kwa nini Luis ?”
“Luis ni Mchezaji wa Al Ahly 🇪🇬 na atacheza hapa, atapata nafasi kama Hamdy na atapata nafasi kama Wachezaji wengine, kila mmoja ni Mchezaji wa Al Ahly, hapa atacheza. Nitamtoa Tau, nitamtoa Sherif na nitamtoa hata Afsha, hapa hakuna star wachezaji wote ni sawa,” amesema Pitso Mosimane.