
Idara ya Uhamiaji imetoa ufafanuzi kuhusu sakata la wachezaji watatu wa Singida Black Stars ambao ni Emmanuel Kwame Keyekeh (Ghana), Josephat Arthur Bada (Cote d’Ivoire), na Muhamed Damaro Camara (Guinea) kupewa uraia wa Tanzania na kubainisha watatu hao ni sasa ni raia wa Tanzania kwa Tajnisi.
Taarifa ya leo Januari 23, 2025 iliyotolewa na Msemaji wa Idara ya Ihamiaji, SSI. Paul J. Mselle imebainisha kwamba wachezaji hao waliomba na kupewa uraia kwa mujibu wa vifungu vya 9 na 23 vya Sheria ya Uraia ya Tanzania, Sura ya 357.


