
OFISA habari na msemaji wa klabu ya Yanga, Hassan Bumbuli na Haji Manara, wamezungumza na wanahabari leo Machi 16, 2022 kuhusiana na suala la mchezaji wao wa Yanga Princess, Aisha Masaka kuuzwa nje ya nchi na kuelekea mchezo wa ligi kuu utakaochezwa Machi 19, 2022.
Aidha wametangaza kuwa kesho Machi 17, 2022 watatembelea hospitali ya Ocean Road na kutoa msaada ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha mwaka mmoja tangu Hayati Magufuli, afariki dunia.
“Kutakuwa na Mechi ya Utangulizi kati ya Wafanyakazi wa Yanga na Wasanii ikiambatana na Burudani Kubwa kutoka kwa Wasanii wakubwa pia Uongozi wa Young Africans SC umemualika Rasmi Mh. Rais Mama yetu Samia Suluhu Hassan kuja kushuhudia mchezo wetu dhidi ya KMC katika kilele cha Mwaka Mmoja wa Urais wake”

⚫️ SIKILIZA + 255 GLOBAL RADIO LIVE: http://ndstream.net/globalradio/ ⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx