×

Vita vya Ukraine: Viongozi wa Ulaya Wapanda Treni Kukutana na Zelensky

Ukraine imepongeza ujasiri wa viongozi wa Ulaya waliosafiri kwa treni kutoka Poland hadi Kyiv kuonesha mshikamano wao baada ya mji huo kushambuliwa na Urusi.

 

Mawaziri wakuu wa Poland, Slovenia na Jamhuri ya Czech walikutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky Jumanne jioni wakati amri ya kutotoka nje ilianza kutekelezwa mjini Kyiv.

Baada ya hapo, kiongozi wa Czech aliwaambia Waukraine kwamba “hawako peke yao”.

 

Kundi hilo la viongozi ni la kwanza kutoka Ulaya kuzuru Ukraine tangu uvamizi wa Urusi.

“Tunafurahia pambano lako la ujasiri,” Petr Fiala aliandika kwenye tweet. “Tunajua kwamba wewe pia unapigania maisha yetu. Hauko peke yako, nchi zetu zinasimama na wewe.”

 

Mateusz Morawiecki wa Poland alisema kuwa Ulaya haitakuwa sawa ikiwa itapoteza Ukraine. Badala yake, aliandika, lingekuwa “toleo lililoshindwa, lililofedheheshwa na la kusikitisha la utu wake wa zamani”

Leave a Comment