
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza kifo cha Spika wa Bunge la Uganda, Jacob Oulanyah leo Jumapili “Alikuwa Kada mzuri nimechelewa kutoa taarifa ili Watoto wake wajulishwe kwanza”.
Kilichosababisha kifo cha Oulanyah hakijabainishwa lakini alikuwa amelazwa Hospitali nchini Marekani kwa zaidi ya mwezi mmoja na ilizua mjadala kwa Waganda ambao walidai iligharimu pesa nyingi sana za walipa kodi kumtibu.
Oulanyah alichukua kiti cha Spika wa Bunge la Uganda mnamo Mei 2021 na kabla ya hapo alikuwa Naibu Spika kuanzia 2011.
20th March, 2022
Countrymen and Countrywomen.
It is with a lot of sadness that I announce the death of the Rt. Hon. Jacob Oulanyah, the Speaker of Parliament.— Yoweri K Museveni (@KagutaMuseveni) March 20, 2022