Rais Samia Awaapisha Mabalozi Wanne Ikulu Dar es Salaam, Awapangia Vituo vya Kazi
Global Publishers April 10, 2022 0 Comments
SHARE THIS:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Balozi Macocha Mosha Tembele kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa (Multilateral Co-operation) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Aprili, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan Leo Aprili 10, 2022 amewaapisha mabalozi wanne Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Mabalozi walioapishwa kutoka kulia Balozi Macocha Mosha Tembele, Balozi Mindi Hellen Kasiga, Balozi Noel Emmanuel Kaganda, Balozi James Gillawa Bwana hafla hiyo iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais Samia akimuapisha Balozi Mindi Hellen Kasiga kuwa Mkurugenzi wa Idara/Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika . Rais Samia akimuapisha Balozi Noel Emmanuel Kaganda kuhudumia Chuo cha Ulinzi (NDC) katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Aprili, 2022.Rais Samia akimuapisha Balozi James Gillawa Bwana kuhudumu katika Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa (Multilateral Co-operation) katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Aprili, 2022.Mabalozi walioapishwa wakila Kiapo cha Uadilifu. Kutoka kulia Balozi Macocha Mosha Tembele, Balozi Mindi Hellen Kasiga, Balozi Noel Emmanuel Kaganda, Balozi James Gillawa Bwana katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.Rais Samia akizungumza na viongozi mbalimbali Ikulu Jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwaapisha Mabalozi 4 Ikulu Jijini Dar es Salaam.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Hussein Kattanga pamoja na Balozi Macocha Mosha Tembele, Balozi Mindi Hellen Kasiga, Balozi Noel Emmanuel Kaganda, Balozi James Gillawa Bwana katika hafla ya uapisho wa Mabalozi hao iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 April 2022.Rais Samia akisalimiana na Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Donald Wright mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Aprili, 2022.Rais Samia Suluhu Hassan, akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Donald Wright.Rais Samia akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Donald Wright mara baada ya mazungumzo yao Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Aprili, 2022.