
WAZIRI wa Ulinzi nchini Norway, Odd Roger Anoksen ‘50’ amejizulu baada ya kubainika amekuwa katika uhusiano wa kimapenzi na binti wa mika 18.
Katika mahojiano na shirika la habari la la NTB, waziri Anoksen alikiri makosa yake akiomba radhi akisema uamuzi wake uliathiri maisha ya wengi.

“Nimefanya maamuzi mabaya kadhaa. Ninaomba msamaha kwani maamuzi yangu yameathiri maisha ya watu wengi,” alisema Anoksen.
Kulingana na vyombo vya habari nchini humo, Anoksen alianza uhusiano wa kimapenzi na mwanamke huyo mwaka wa 2005 wakati binti huyo akiwa angali mwanafunzi.