×

Basi la Super Feo Lapata Ajali Tunduru, Ruvuma… Dereva Halima Adaiwa Kukatika Mkono

 

Basi la Super Feo linalofanya safari zake Songea – Dar kupitia njia ya Lindi limepata ajali asubuhi ya leo Jumapili Mei 22, 2022 katika eneo la Kijiji cha Hulia Wilaya ya Tunduru na kusababisha majeruhi kadhaa akiwemo Dereva Halima Mbwana ambaye amedaiwa kukatika mkono.

 

Halima, mama wa watoto watatu, alipata umaarufu hivi karibuni kwa kuwa ni dereva wa kike anayeendesha basi la abiria aliyeanzia kuwa kondakta kabla ya kwenda kusomea udereva, amekimbizwa hospitali kwa matibabu zaidi

Kamanda wa Polisi Ruvuma, Joseph Konyo amekiri kutokea kwa ajali hiyo na kusema atatoa taarifa kamili baadaye.

YAMOTO BAND MPYA Wafunguka MAZITO, Kuwarithi MBOSSO, ENOCK, BEKA NA ASLAY | DSM FLEVA..

Leave a Comment