×

Breaking: Ajali Yaua Watu 18 Mafinga Iringa, Coaster Yagongana Uso kwa Uso na Lori

Taarifa zilizotufikia hivi punde ni kuwa watu 18 wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya gari aina ya Toyota Coaster kugongana uso kwa uso na lori la mizigo karibu na eneo la Changarawe, Mafinga mkiani Iringa leo Juni 10, 2022.

 

Akithibitisha kutokea ajali hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, ACP Allan Bukumbi amesema ajali imesababisha vifo zaidi ya 10 akisema kuwa taarifa ziaidi zitatolewa baadaye

 

“Ni kweli ajali imetokea na inasadikika watu zaidi 10 wamepoteza maisha papo hapo,” amesema.

Leave a Comment