Washindi wa Wiki ya Kwanza wa Vodacom M-Pesa Imeitika Wapatikana Arusha
Global Publishers August 14, 2022 0 Comments
SHARE THIS:
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya jiji la Arusha, Selemani Msumi akimkabidhi funguo mshindi wa Bajaj wa promosheni ya Vodacom “M-Pesa Imeitika” kutoka Morombo jijini Arusha, Mwanaisha Nyonyo Mohamed wakati wa hafla ya wiki ya kwanza iliyofanyika kwenye viwanja vya soko la kilombero jijini humo. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Kanda ya Kaskazini Abednego Mhagama. Vodacom inatoa zawadi ya bajaj moja na Bodaboda nne (zote mpya) kila wiki kwa wiki nane ili kuhamasisha matumizi ya pesa kidijitali. Ambapo zawadi kuu itakuwa ni nyumba mpya iliyosheheni samani zote. Washindi waliojishindia bodaboda kwenye promosheni ya Vodacom “M-Pesa Imeitika” wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao. Vodacom inatoa zawadi ya bajaj moja na Bodaboda nne (zote mpya) kila wiki kwa wiki nane ili kuhamasisha matumizi ya pesa kidijitali. Ambapo zawadi kuu itakuwa ni nyumba mpya iliyosheheni samani zote.