×

Korea Kaskazini Yafanya Majaribio Mawili ya Makombora, Korea Kusini Yataka Diplomasia

 

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un

RAIS wa Korea Kusini Yoon Suk-Yeol atoa wito wa kuwepo kwa diplomasia yenye lengo la kujenga amani endelevu kati ya wapinzani hao huku kukiwa na mvutano kuhusu mpango wa kuendeleza silaha wa Korea Kaskazini.

 

Akizungumza katika mkutano na wanahabari siku ya Jumatano, Bw Yoon alisema hataki mabadiliko ya kisiasa nchini Korea Kaskazini ambayo yameletwa kwa nguvu na akahimiza Kaskazini kurejea kwenye mazungumzo yanayolenga kubadilishana hatua za kuondoa silaha za nyuklia kwa manufaa ya kiuchumi.

Rais wa Korea Kusini Yoon Suk-Yeol

Wito wa mazungumzo unakuja licha ya vitisho vilivyotolewa na dadake Kim Jong Un huku akilaumiwa kwa vipeperushi vya propaganda kutoka Korea Kusini vilivyopatikana karibu na mpaka kwa kusababisha milipuko ya Covid-19.

Makombora yaliyorushwa na nchi ya Korea Kaskazini siku ya Jumatano

Makombora hayo yalirushwa kutoka mji wa pwani ya magharibi wa Onchon mapema Jumatano, chanzo cha jeshi la Korea Kusini kilisema.

 

Imeandikwa:Dunstan Mtili Erick Kwa msaada wa mitandao

Leave a Comment