×

Kampuni ya Kompyuta ya Dell ya Marekani Yasitisha Rasmi Huduma Zake Nchini Urusi

Kampuni ya Dell imesitisha rasmi huduma zake nchini Urusi

KAMPUNI ya teknolojia ya Dell yenye Makao yake Makuu nchini Marekani inasema ilikuwa imemaliza shughuli zote nchini Urusi baada ya kufunga ofisi zake mapema mwezi huu, na kuwa kampuni ya mwisho kutoka Ulaya kuondoka nchini baada ya Urusi kufanya uvamizi nchini Ukraine.

 

Kampuni ya kompyuta ya Marekani ya Dell ndio msambazaji mkuu wa seva nchini Urusi.

 

Kampuni hiyo ilisitisha mauzo nchini Ukraine na Urusi mnamo Februari mwaka huu huku ikifuatilia hali ilivyo ili kubaini hatua zake zinazofuata.

 

Msemaji wa kampuni ya Dell, Mike Siemienas aliiambia Reuters “Mwezi Februari, tulifanya uamuzi wa kutouza, kutoa huduma, au kusaidia bidhaa nchini Urusi, Belarusi, na mikoa ya Donetsk na Luhansk ya Ukraine, pamoja na Crimea ambayo tayari imewekewa vikwazo,”

Kampuni ya Dell

Shirika la habari la TASS linaloendeshwa na serikali lilimnukuu Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Vasily Shpak akisema, “Tunafuatilia maendeleo ya hali hiyo.”

 

Aliongeza kusema “Kulingana na data zetu, idadi kubwa ya wataalamu wa kituo cha R&D cha Dell na wahandisi wa usaidizi huko St. Petersburg na Moscow tayari wamepokea ofa za kazi na malipo ya ushindani kutoka kwa wazalishaji wa Urusi”.

 

Imeandaliwa na Simon Molanga kwa msaada wa mtandao.

 

Leave a Comment