×

Shujaa wa Hoteli ya Rwanda Atua Qatar Baada ya Kuachiliwa Huru

Paul Rusesabagina, ambaye aliigiza kama shujaa katika filamu ya Hollywood Hotel Rwanda, amewasili Qatar baada ya kuachiliwa kutoka jela nchini Rwanda.

Afisa wa Ikulu ya Marekani alisema Rusesabagina aliondoka Rwanda siku ya Jumatatu na kufika katika mji mkuu wa Qatar, Doha.

“Naweza kuthibitisha kwamba Paul Rusesabagina ameondoka Rwanda na kwa sasa yuko Doha,” mratibu wa Baraza la Usalama la Kitaifa la Marekani John Kirby amenukuliwa akisema.

“Hivi karibuni atarejea Marekani na familia yake, kwa vile nina hakika hakuna anayeshangaa, wana hamu ya kumkaribisha tena hapa nyumbani.”

Mazungumzo yaliyosimamiwa na Qatar yalipelekea kuachiliwa kwake kutoka gerezani mwishoni mwa juma – miaka miwili baada ya kuhukumiwa miaka 25 kwa ugaidi.

Wafuasi wake waliita kesi hiyo kuwa ya udanganyifu. Adhabu hiyo ilibadilishwa kwa amri ya rais, kulingana na msemaji wa serikali.

Ilifuata miaka ya shinikizo la kidiplomasia na Marekani, ambapo Rusesabagina alikuwa akiishi tangu 2009.

Bw Rusesabagina anasifiwa kwa kuokoa watu 1,200 wakati wa mauaji ya kimbari ya 1994 nchini Rwanda.

#EXCLUSIVE: ”KWENYE USAJILI TUMEPIGWA” – MO DEWJI AFUNGUKA SABABU ya KUKWAMA NUSU FAINALI | PART 3

Leave a Comment