
Papa Francis ametoa wito kwa waliojeruhiwa huko Gaza kuhudumiwa mara moja na misaada zaidi ya kibinadamu iruhusiwe kuingia katika eneo hilo.
Akizungumza kutoka Jiji la Vatican katika sala yake ya kila wiki ya Malaika wa Bwana, Papa alisema fikra zake kila siku zinaelekea katika “mateso” na “hali mbaya” katika Israeli na maeneo ya Palestina.
“Naomba waliojeruhiwa huko Gaza wasaidiwe mara moja. Raia wanapaswa kulindwa, na misaada zaidi ya kibinadamu inapaswa kuwasilishwa kwa watu hao waliochoka,” Papa aliongeza.
Papa Francis pia alitoa wito mateka waliochukuliwa na Hamas kutoka Israel tarehe 7 Oktoba waachiliwe.