×

Rais Samia azungumzia vipaumbele vya Tanzania aliposhiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) unaojadili masuala ya Tabianchi na Usalama wa Chakula, Ngurdoto Mkoani Arusha tarehe 23 Novemba, 2023

Rais Samia Suluhu Hassan azungumzia baadhi ya vipaumbele vya Tanzania aliposhiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) unaojadili Masuala ya Tabianchi na Usalama wa Chakula Mkoani Arusha.

Rais Samia amesema kuwa lengo la kutunza mazingira ili kupunguza umaskini katika nchi za Afrika Mashariki kwa kutumia mazingira kama moja ya chanzo cha mapato.

Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamud pamoja na wageni mbalimbali wakifuatilia kwa makini wakati Viongozi mbalimbali walipokuwa wakizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) unaojadili masuala ya Tabianchi na Usalama wa Chakula, Ngurdoto Mkoani Arusha tarehe 23 Novemba, 2023
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Rais wa Burundi Mhe. Évariste Ndayishimiye pamoja na Rais wa Kenya Mhe. William Ruto wakati wa Wimbo wa Taifa wa Tanzania ukiimbwa kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) unaojadili kuhusu masuala ya Tabianchi na Usalama wa Chakula, Ngurdoto Mkoani Arusha tarehe 23 Novemba, 2023

Leave a Comment