
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amekutana na Balozi wa Qatar nchini Fahad Rashid Al Muraikhi.
Pia Majaliwa amepokea salamu za pole kutoka Serikali ya Qatar kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Ali Hassan Mwinyi.
Mazungumzo hayo yamefanyika Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam Machi 8, 2024.

