×

Rais Samia Atunuku Nishani Za Miaka 60 Muungano Na Kuzindua Kitabu – (Picha +Video)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mama Janeth Magufuli Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo aliipokea kwa niaba ya Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024. Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hutunukiwa kwa Wakuu wa Nchi Wastaafu (hai au marehemu) wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walioingia madarakani kwa njia ya kikatiba na wameendelea kuonesha Maadili mema yenye nidhamu, heshima na mfano wa kuigwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan Aprili 24, 2024 atoa Nishani za Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuzindua Kitabu cha Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais katika Viwanja vya Ikulu – Chamwino Dodoma.

Rais Samia akimkabidhi Mama Salma Kikwete Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo aliipokea kwa niaba ya Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais Samia akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Makamu Rais Mstaafu Mohamed Gharib Bilal.
Rais Samia  akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, John Samwel Malecela.
Rais Samia akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick.

Leave a Comment