
Viongozi na wachezaji wa Klabu ya Yanga, leo wametinga bungeni jijini Dodoma kwa mwaliko wa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro.
Wakiwa bungeni, Naibu Spika, Mussa Azan Zungu aliwatambulisha ambapo wabunge walilipuka kwa shangwe wakiwapigia makofi kwa nguvu.
