
Rais Samia Suluhu Hassan ameiagiza Wakala wa Taifa wa Uhifadhi wa Chakula (NFRA) kuanzia kesho Julai 18, 2024 ianze kununua mahindi kilo moja kwa shilingi 700/- kutoka bei aliyoitangaza akiwa mkoani Katavi ya shilingi 600/-.
Ametoa agizo hilo wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa CCM wa Nelson Mandela mkoani Rukwa.

Rais Samia amesema ametangaza bei hiyo mpya kutokana na maombi ya wakulima akisema huo ndio usikivu wa serikali.
“Kuna maombi yametoka hapa, nimepokea malalamiko nikiwa Katavi nikiwa kule nikapandisha bei (mia sita), nimekuja Rukwa malalamiko bado ni bei, nakuagiza waziri nendeni na bei ya mia saba. NFRA kuanzia kesho nunueni mahindi kwa mia saba… Ndugu zangu na huo ndio usikivu wa serikali,” amesema Rais Samia.

