×

Hali ya Daraja la Somanga, Mtama wilayani Kilwa mkoani Lindi – Picha

Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega amerejea tena Somanga asubuhi ya leo ya Aprili 17, 2025 kuendelea na usimamizi wa ukarabati wa daraja la muda ili kuhakikisha wasafiri wanaendelea na safari zao bila kikwazo mara baada ya usiku wa jana wa tarehe 16 Aprili , 2025 eneo la Somanga Mtama na Matandu mkoani Lindi kujaa tena maji na kufunga mawasiliano ya barabara kutoka Dar es Salaam kuelekea mikoa ya Kusini.

Hali ya Daraja la Somanga- Mtama wilayani Kilwa mkoani Lindi likitengenezwa baada ya daraja hilo kukatika jana majira ya asubuhi Aprili 16, 2025 na kulazimika usafiri kusitisha kwa muda kwa wasafiri wanaotoka na kwenda Mikoa ya Kusini pamoja na Dar es Salaam.