
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 27 Juni 2025, amewasili katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma, ambapo alipokelewa kwa heshima ya kitaifa na kukagua gwaride maalum.
Baada ya ukaguzi wa gwaride, Rais Samia alielekea katika Ukumbi wa Bunge ambako anahutubia kikao maalum cha Bunge na kufunga rasmi shughuli za Bunge la 12, kufuatia kuhitimishwa kwa muhula wake wa mwisho wa uendeshaji wa Bunge hilo.
