Mwili wa Marehemu Halima Nassor Ulivyofikishwa Nyumbani Kwake, Kigamboni

Na Bakari H. Mahundu
Mwili wa Marehemu Halima Idd Nassor ulivyofikishwa nyumbani kwake Kibada, Kigamboni Dar es Salaam kwaajili ya dua maalumu nyumbani hapo kabla ya kuzikwa leo Januari 18, 2026 saa 10 jioni katika makaburi ya Kibada kwa Dole Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Marehemu Halima Idd Nassor amefariki dunia leo Januari 18, 2026 katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
Waombelezaji mbalimbali wakiwemo viongozi wa Kiserikali wamewasili Kibada, Kigamboni Dar es Salaam nyumbani kwa Marehemu Mheshimiwa Halima Idd Nassor kutoa pole na kufariji ndugu na familia ya Halima.


