
Staa wa muziki na filamu Bongo, Lulu Diva (@luludivatz), ameibua gumzo kubwa mitandaoni baada ya kuonyesha kiwango kipya cha kujiamini na kujikubali, hali iliyowafanya mashabiki wake kushindwa kuficha hisia zao.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Story, Lulu alijisitiri kwa mvuto na bashasha huku akiambatanisha picha zake zenye kuonyesha umbo lake la kuvutia, jambo lililoibua maoni mengi kutoka kwa wafuasi wake.
Katika hali ya utani uliochanganyika na mahaba, Lulu aliandika:
“Hey Sexy Lady… 😋♥️ Unaniitaje… 🤷🏽♀️
A) LULU DIVA
B) DIVANA
C) Sexy Diva”
Ujumbe huo uliwafanya mashabiki kuingia “mtego” wa majibu, wengi wakimiminika kwenye DM na comments wakimsifia kwa uzuri na kujiamini kwake.
Kana kwamba haitoshi, Lulu aliendelea kuongeza ladha zaidi kwa kuandika:
“Candy 🍭 shop Bebe 🥰♥️💛”
Kauli hiyo ya utani iliongeza joto la mjadala, huku baadhi wakisema staa huyo anajua kucheza na hisia za mashabiki wake, na wengine wakimtaja kama “malkia wa confidence”.
Kwa muda sasa, Lulu Diva ameonekana kubadilika kimtazamo, akionyesha wazi kufurahia maisha yake, mwonekano wake na kutuma ujumbe wa kujipenda, kujiamini na kutokujali maneno ya watu.
