
Dar es saalam, Tanzania – Kampuni ya Kerry Group imezindua ripoti ya Kenya Taste Charts 2026, ikionyesha mabadiliko makubwa katika chaguo za ladha za watumiaji barani Afrika. Ripoti hiyo inahusisha nchi 78, zikiwemo Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda na Zambia.
Ripoti inaonesha kuwa watumiaji wengi barani Afrika wanahama kutoka ladha za kawaida za vyakula vya msingi na kuelekea ladha zenye mchanganyiko mpana, maalum zaidi, zenye utofauti mkubwa na uzoefu unaofanana na ule wa “cocktail” katika vyakula na vinywaji vya kila siku.
Ripoti ya Taste Charts 2026 imetayarishwa na zaidi ya wataalamu 1,200 wa sayansi, wabunifu wa ladha 100, wataalamu 70 wa sanaa ya chakula, pamoja na wataalamu 250 wa masoko na uchambuzi wa mwenendo wa watumiaji.
Mabadiliko ya ladha barani Afrika
Kadiri matarajio ya watumiaji yanavyozidi kubadilika, Taste Charts 2026 imepanua makundi yake kutoka matano hadi saba. Makundi hayo ni: vinywaji vya viburudisho, pombe na ladha zinazochochewa na pombe, chai, kahawa na kakao, vitafunwa vyenye chumvi, vyakula vitamu, supu na virutubisho, pamoja na nyama, milo kamili na lishe.

Mtazamo huu unaonyesha kuwa starehe, afya, mila, mitindo mipya, pamoja na ushawishi wa kimataifa na utambulisho wa ndani, vinaendelea kuathiri maamuzi ya ladha za watumiaji.
“Tunachokiona ni mabadiliko ya msingi katika namna watumiaji barani Afrika wanavyotumia vyakula na vinywaji. Kuna mwelekeo wa kuhama kutoka ladha za kawaida kwenda kwenye uzoefu maalum wenye tabaka nyingi za ladha,” alisema Regis Manyange, Mkurugenzi wa Biashara Afrika Mashariki wa Kerry Group.
Aliongeza kuwa kupitia jukwaa la kidijitali KerryNow™, wateja wanawezeshwa kupata ladha mpya, kuagiza sampuli na kuharakisha ubunifu wa bidhaa kulingana na mabadiliko ya soko.
Mwelekeo wa ladha mahususi.
Matunda yanaendelea kuongoza ubunifu wa vinywaji, huku mahitaji ya ladha halisi yakiongezeka. Ladha za asili kama machungwa na limao bado zinaongoza, lakini aina mpya za kisasa zinaibuka kwa kasi.
• Rwanda, Uganda na Zambia – tangawizi inaongezeka kwa kasi katika vinywaji
• Tanzania – ukwaju unaibuka kama ladha mpya inayopata umaarufu
• Kenya – mchanganyiko wa tamu na kali (Swicy) unaongoza, hasa kwenye vinywaji vinavyochochewa na ladha za pombe kama Mango Chilli
Mwelekeo huo pia unaonekana katika vitafunwa vyenye chumvi, ambapo pilipili ya kawaida inabadilika na kuwa mchanganyiko wa viungo wenye tabaka nyingi za ladha.
Ukali wenye tabaka na athari za vinywaji
Watumiaji wanahama kutoka ukali wa aina moja na kuelekea ladha zenye mchanganyiko wa viungo. Barani Afrika, matumizi ya viungo vinavyotokana na paprika yanaongezeka, yakitoa ladha na harufu inayochochewa na utamaduni wa vyakula vya mitaani.
Kuibuka kwa ladha ya “Swicy”
Mchanganyiko wa ladha tamu na kali unaendelea kupata umaarufu. Kenya inaongoza katika ubunifu wa ladha hizi, hasa kwenye vinywaji vinavyochochewa na ladha za pombe. Mwelekeo huo pia unaonekana katika vitafunwa vyenye chumvi, ambako viungo vinachanganywa ili kutoa ladha yenye kina zaidi.
Athari ya “Mocktail”
Ladha zinazotokana na vinywaji vya pombe zinaongezeka katika vinywaji visivyo na pombe.
• Mojito inaongezeka Tanzania na Rwanda
• Piña Colada inakua kwa kasi Uganda na Zambia
Kubadilisha maarifa kuwa vitendo
Ripoti ya Taste Charts 2026 inaungwa mkono na jukwaa la kidijitali KerryNow, linalowawezesha wateja kupata orodha ya ladha, kuagiza sampuli na kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu wa Kerry Group.
Kwa taarifa zaidi, wasomaji wanashauriwa kusoma ripoti kamili iliyotolewa na kampuni hiyo.