×

Trump Aionya Iran: Shambulio kwa Meli Litajibiwa kwa Kushambulia Miundombinu

Rais wa Marekani, Donald Trump.

Rais wa Marekani, Donald Trump, ametoa onyo kali kwa Iran akisema Marekani itajibu kwa mashambulizi ya moja kwa moja dhidi ya miundombinu ya nchi hiyo ikiwa Tehran itashambulia meli zinazopita katika Mlango wa Hormuz.

Trump alisema kuwa iwapo Iran itatumia makombora, ndege zisizo na rubani (drones), roketi au silaha nyingine yoyote kushambulia meli za kibiashara katika eneo hilo, Marekani itashambulia na kuharibu daraja au kituo cha kuzalisha umeme cha Iran kwa kila shambulio litakalofanywa.

Aidha, alisisitiza kuwa mashambulizi hayo yanaweza kulenga miundombinu iliyopo ndani au karibu na mji mkuu wa Iran, Tehran.

Kauli hiyo imeongeza mvutano kati ya Marekani na Iran huku Mlango wa Hormuz ukiendelea kuwa njia muhimu ya usafirishaji wa mafuta duniani.

Leave a Comment