
Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Harmonize, ameachia rasmi wimbo wake mpya unaoitwa “Love Design” akimshirikisha rapa Darassa, Julai 24, 2026.
Wimbo huo ni wa mahadhi ya Bongo Flava/Romantic Afro-pop, ukiwa umejikita katika simulizi la mapenzi linaloelezea jinsi wapenzi walivyounda msingi na mfumo maalum wa kulinda, kuenzi na kudumisha uhusiano wao.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmonize maarufu kama Konde Boy, amesema Love Design ni mwanzo wa mfululizo wa nyimbo mpya atakazoziachilia kuelekea uzinduzi wa albamu yake mpya inayotarajiwa kutoka hivi karibuni.
Hii si mara ya kwanza kwa Harmonize na Darassa kushirikiana, kwani tayari wamewahi kufanya kazi pamoja kwenye nyimbo zilizopata mafanikio makubwa ikiwemo “Mazoea” iliyotoka mwaka 2024 pamoja na “Yumba”, ushirikiano ambao ulipokelewa vizuri na mashabiki wa muziki wa Bongo Fleva.