Mwigizaji mkongwe wa filamu Bongo, Vincent Kigosi, maarufu kama Ray, amefichua kuwa mzazi mwenzake, Chuchu Hansy, anatarajia kupata mtoto wao wa pili.
Ray ametoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram, akieleza furaha na shukrani alizonazo moyoni kutokana na ujio wa mtoto huyo, huku akimshukuru Mungu kwa baraka hiyo katika familia yao.
Katika ujumbe wake, Ray ameandika:
“MY LOVELY MZUNGU, maneno hayatoshi kueleza furaha na shukrani nilizonazo moyoni. Unakaribia kunipa zawadi ya thamani kuliko zote, mtoto wetu wa pili.
Namshukuru Mungu kwa ajili yako na kwa baraka hii kubwa katika familia yetu.
Asante kwa upendo wako na kwa kunipa furaha isiyo na kipimo. Nakupenda sana MY LOVELY MZUNGU. Mungu ailinde familia yetu na abariki familia yetu daima.
Nakuahidi kuthamini familia yetu, kukupenda sana na kusimama na wewe katika kila hatua ya maisha yetu.”

Ray pia ametumia ujumbe huo kuwashukuru watu mbalimbali waliohusika katika maandalizi ya picha zao, huku akiwataja wauzaji wa mavazi pamoja na mpiga picha.
Ujio wa mtoto huyo unakuwa hatua nyingine katika maisha ya familia ya Ray na Chuchu Hansy, huku mashabiki wao wakituma pongezi na kuwatakia safari njema kuelekea kumpokea mtoto wao wa pili.
Ray ni miongoni mwa waigizaji waliodumu kwa muda mrefu katika tasnia ya filamu Tanzania na amejijengea jina kubwa kupitia kazi zake mbalimbali katika Bongo Movies.
