
Droo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League) msimu wa 2026/27 inafanyika leo, Alhamisi Agosti 27, 2026, mjini Monaco, ambapo timu 36 zitajua wapinzani wao katika hatua ya ligi.
Droo hiyo itaanza majira ya saa 1:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki, huku mashindano yakiendelea kutumia mfumo mpya ambao umeondoa makundi ya kawaida yenye timu nne.
Katika mfumo huo, timu zote 36 zitakuwa kwenye ligi moja, ambapo kila klabu itacheza jumla ya michezo minane dhidi ya wapinzani tofauti. Kila timu itakutana na timu mbili kutoka kila moja ya pot nne za upangaji.
Miongoni mwa vigogo waliopo kwenye droo hiyo ni Real Madrid, Barcelona, Liverpool, Manchester City, Arsenal, Bayern Munich, Paris Saint-Germain, Inter Milan na Atlético Madrid, ambao wamewekwa kwenye Pot 1.

Pot 2 ina timu kubwa kama Manchester United, Borussia Dortmund, Roma, Porto, Aston Villa na PSV, wakati Pot 3 ikiwa na Napoli, RB Leipzig, Villarreal, Galatasaray na Fenerbahçe.
Kwa upande wa Pot 4, timu zinazotarajiwa kushiriki droo hiyo ni pamoja na Stuttgart, LASK, Como, Lens na Slavia Prague.
Michezo ya hatua ya ligi ya Champions League inaanza Septemba 8, 2026, huku ratiba kamili ya kila timu ikitarajiwa kutolewa kabla au ifikapo Agosti 29.
Fainali ya msimu huu imepangwa kufanyika katika Uwanja wa Estadio Metropolitano, Madrid, Hispania, Juni 5, 2027.
Droo hiyo inatarajiwa kuvuta hisia kubwa kutokana na uwezekano wa vigogo kama Real Madrid, Liverpool, Barcelona, Arsenal na Manchester City kukutana na ratiba ngumu mapema katika safari yao ya kuwania ubingwa wa Ulaya.
Na Ashura Karimu, DSJ.