×

Wasira Akutana na Wabunge wa CCM katika Makao Makuu ya Chama

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM – Bara), Stephen Wasira, amekutana na kuzungumza na Kamati ya Wabunge wa CCM, Septemba 2,  2026, katika Ukumbi wa White House Makao Makuu ya Chama jijini Dodoma.

Katika kikao hicho Wasira aliambatana na ujumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM ukiongozwa na Katibu Mkuu, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro.

Leave a Comment