×

Sevilla Kuikabili Valencia, Nani Kuibuka na Ushindi?

Klabu ya Sevilla itakuwa mwenyeji wa Valencia katika mchezo wa raundi ya tano ya LALIGA msimu wa 2026/27, utakaopigwa kwenye Uwanja wa Ramón Sánchez-Pizjuán. Mchezo huo unatarajiwa kuanza saa 22:00 jioni.

Sevilla inaingia kwenye mchezo huo ikiwa na pointi saba baada ya kucheza michezo minne, ikiwa imeshinda michezo miwili, sare moja na kupoteza mmoja. Timu hiyo ilianza msimu kwa ushindi dhidi ya Rayo Vallecano na Athletic Bilbao, kabla ya kufungwa na Atletico Madrid na kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Espanyol.

Kwa upande wa Valencia, hali ni tofauti baada ya kuanza msimu kwa kusuasua. Wakiwa na pointi moja pekee, Valencia wako nafasi ya mwisho baada ya sare moja na vipigo vitatu, huku wakifunga bao moja tu na kuruhusu mabao tisa. Kipigo cha mwisho cha 5-0 dhidi ya Barcelona kimeongeza presha kwa kocha Carlos Corberán.

Kocha Corberán mwenyewe alikiri hali hiyo baada ya mechi, akisema kwamba dhidi ya timu kubwa kama Barcelona, kila kitu lazima kiende sawasawa ili kupata matokeo mazuri, jambo ambalo halikutokea kwao siku hiyo.

Kwa sasa Valencia wanaingia kwenye mchezo huu wakiwa hawana ushindi katika mechi michezo minne, huku baadhi ya ripoti zikieleza kuwa wana changamoto kubwa ya majeruhi kambini kwao.

Meridianbet inasema kuna michezo kama Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli. Ingia katika kasino ya mtandaoni ya Meridianbet na ujiokotee mkwanja mapema.  Jiunge sasa au Tembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Sevilla pia itakosa baadhi ya wachezaji muhimu. Arouna Sangante hatacheza kutokana na kadi nyekundu aliyopata dhidi ya Espanyol, huku Rubén Vargas akiwa nje kutokana na majeraha. Valencia nayo ina changamoto kubwa za majeraha, akiwemo Mouctar Diakhaby, ambaye ameongezeka kwenye orodha ya wachezaji wanaokosekana.

Kwa ujumla, mchezo huu unatarajiwa kuwa muhimu kwa kila timu. Sevilla itatafuta pointi tatu mbele ya mashabiki wake ili kuendelea kupanda kwenye msimamo, wakati Valencia itahitaji matokeo mazuri ili kuondokana na mwanzo mbaya wa msimu. Historia ya hivi karibuni inaibeba Valencia matumaini, kwani Sevilla haijaifunga katika mechi sita zilizopita kati yao.

Leave a Comment