The House of Favourite Newspapers

Sanch: Nikizaa, Situpii za Utupu!

Na Imelda Mtema | RISASI | HABARI FUPIFUPI

MREMBO mwenye fi ga matata Bongo, Jane Rimoy ‘Sanch’ amefunguka kuwa akibahatika kupata mtoto hataonekana akijiachia tena nusu utupu kwenye mitandao ya kijamii.

Sanch alisema kutokana na kupenda kutupia picha zinazomuonesha vyema umbo lake katika mitandao ya kijamii, siku akizaa hataonekana tena huko kwa sababu atakuwa anamfundisha mwanaye tabia isiyo njema.

“Unajua ukishakuwa mama unatakiwa ujiheshimu na mambo ya kiujana uachane nayo hivyo siku nikizaa tu na mambo ya kujiachia kihasara mitandaoni ndiyo yataishia hapo ili nimlinde mwanangu kimaadili kwani sipendi aige maisha yangu haya ninayopenda kuishi ya ujana,” alisema Sanch.

Comments are closed.