×

Shinda Nyumba Yawaibukia Wasomaji wa Tegeta na Viunga Vyake

Aisha Ajibu kushoto, Mr. Shinda Nyumba, Hawa Ajibu na Mama Mrangi wakiwa kwenye pozi.

 

Wasomaji wa magazeti ya Global Publishers ambayo ni Amani, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Risasi, Uwazi, na Championi wa pande za Tegeta na viunga vyake jana Alhamisi, waliibukiwa na Mr. Shinda Nyumba aliyekuwa na timu nzima ya promesheni ya Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba.

 

Ofisa Usambazaji wa Global Publishers, Jimmy Haroub (kushoto) akimuelekeza Benjamin Chimenya kuzaja kuponi wakati kulia ni Jackson Aloyce akigonga supu.

 

Mr. Shinda Nyumba akiwa na timu yake walianzia Njia ya Panda ya Kunduchi (Mbuyuni) kunadi gazeti la Amani sambamba na magazeti mengine ya Global yenye kuponi ambayo msomaji alitakiwa kununua gazeti, kuijaza na kuikata kuponi kisha kuipa timu ya msafara huo.

 

 

Wasomaji hao walionesha furaha yao kwa msafara huo na kuanza kuchangamkia gazeti la Amani ambalo linakuwa mtaani kila Alhamisi na kujaza kuponi kila mmoja akijaribu bahati yake kuweza kujishindia nyumba mpya na samani zake ndani hiyo na zawadi zingine ikiwemo simu za kisasa ‘smart phone’, ving’amuzi vya Ting, Dinner Set na pikipiki.

 

Mr. Shinda Nyumba na wasomaji.

 

Baada ya kuagana na wasomaji hao msafara huo ulielekea maeneo ya Tegeta hadi Bunju na viunga vyake, kisha ukaenda kumalizia mzunguuko wake eneo la kiwanda cha saruji cha Wazo Hill ambapo umati wa wasomaji waliokutwa eneo hilo walianza kuchangamkia magazeti hayo.

 

Fadhili Kimwaga wa Tegeta akiwa na Magazeti ya Global Publishers

Baadhi ya wasomaji hao walionekana kuvutiwa na muonekano wa Mr Shinda Nyumba na kuamua kupiga nae picha za Selfie kwa ajili ya kumbukumbu zao.

Kimwaga akitumbukiza kuponi

 

Hawa Maulid (Kulia) na Aisha Ajibu wakisoma kwa makini Gazeti la Amani.

 

Na Richard Bukos

Leave a Comment