×

Timu Zaweka Rekodi La Liga

LIGI Kuu ya Hispania, La Liga, inaendelea ku­tikisa huku kila timu ikionyesha kiwango cha hali ya juu uwanjani.

Wikiendi iliy­opita haikuwa mbaya sana kwa kuwa timu nyingi vigogo ziliendelea kupa­ta ushindi jambo ambalo liliifanya ligi hiyo kuendelea na utawala uleule.

 

Barcelona tayari wamejijengea mi­liki kwenye ligi hiyo wakiwa kileleni kwa sasa tofauti ya pointi nne dhidi ya Valen­cia ambao wa­nashika nafasi ya pili.

 

Lakini aja­bu ni k w a m b a pamoja na Real Ma­drid kuibuka na ushindi kwenye mchezo wake wa wikien­di, Barcelona im­ewaacha kwa pointi nane, jambo ambalo linaonekana kuwa gumu sana kwao kuamini kuwa wa­naweza kufanya vizuri msimu huu.

 

Staa wa Barcelona, Lionel Messi ameendelea kutawala kwenye cha­ti ya ufungaji kwenye ligi hiyo na Ulaya kwa ujumla baada ya kufani­kiwa kufunga mabao 12, hadi sasa kwenye ligi huku akiwa hana up­inzani mkubwa kutokana na Cris­tiano Ronaldo ambaye amekuwa akifanya vizuri kwa miaka kadhaa iliyopita kupotea na hadi sasa ana mabao mawi­li tu kwenye ligi hiyo.

L a Liga ya msimu huu ime­onekana k u w a tofauti kidogo k u t o ­k a n a na hadi sasa timu tatu kuwa hazija­p o t e ­z a mche­zo wow­o t e jam­b o am­b a ­l o lime­kuwa halito­k e i k w e n y e ligi hiyo mis­imu mingi iliyo­pita.

 

Hali hii inaonye­sha kuwa upinzani kwa sasa umeongezeka kwenye ligi hiyo, kwa kuwa pia timu nyingi ambazo zilikuwa hazipewi nafasi ya kuwika ndizo zime­onekana kuchukua nafasi mbili za juu.

Timu ya Barcelona haijapoteza mch­ezo wowote, lakini ajabu ni kwamba inalingana na Atletico Madrid pamoja na Valencia, ambazo zote zimesh­acheza michezo 11 bila kupoteza.

Wachambuzi wa masuala ya soka la Hispania wanaamini kuwa kuna uwezekano mkubwa kukawa na ma­badiliko kwenye msi­mamo wa ligi hiyo mwishoni mwa msimu huu to­fauti na hali ili­vyokuwa mis­imu iliyopita.

Hii ni mara ya k w a n z a k weny e l i g i h i y o t i m u kucheza m i c h e z o mingi nam­na hiyo bila k u f u n g w a hata mmoja ndani ya mi­aka 20 iliyo­pita.

 

W e n g i wana amini k u w a kuna ma­b a d i l i k o makubwa j a m b o a m b a l o limechangia Madrid kuonekana kuwa chini kwa sasa tofauti na hali ilivyokuwa hapo nyuma.

Barcelona wenyewe tayari wameshatishia kwenye ligi hiyo wakiwa wameshinda michezo nane na kutoka sare michezo mi­tatu na ndiyo timu inayopewa na­fasi kubwa ya kufanya vizuri kwa msimu huu.

Hata hivyo, kwa Atletico wenyewe hili siyo jambo la ajabu kwa kuwa ni mara ya tatu kwa sasa wanacheza michezo 11 bila kufungwa, walifanya hivyo msimu wa 1996/97 na 1982/83.

 

Mara ya mwisho kwa ligi hiyo kuwa na timu tatu ambazo hazijafungwa baada ya michezo 11 ilikuwa msimu wa 1996/97, wakati Barcelona, Real Madrid na Deportivo zilipocheza michezo 12.

“Hatuna presha kubwa, hili ni jam­bo la kawaida na linaweza kutokea, sisi kukosekana kwenye timu hizo tatu ni mabadiliko ya ligi na wala siyo kitu kinachoweza kutusumbua sana.

 

“Ni vizuri kwa kuwa tunafanya vitu vyetu kwa mpangilio mzuri na tunaamini kuwa mwisho wa msimu ndiyo kila kitu kitakuwa wazi,” alisema beki na nahodha wa Real Madrid, Ser­gio Ramos.

Hofu kubwa ipo kwa Madrid ambao kwenye michezo hiyo 11 wamesha­poteza miwili lakini wakiwa na sare mbili matokeo ambayo siyo mazuri sana kwao kwa msimu huu.

Leave a Comment