×

FT: Yanga 5-0 Mbeya City Uwanja Wa Uhuru, Ligi Kuu

Kikosi cha timu ya Yanga.

FT:  Yanga 5-0 Mbeya City

Dakika ya 90: Zinaongezwa dakika 3 za nyongeza.

Dakika ya 85: Mashabiki wa Yanga wanaongeza kasi ya kushangilia.

Dakika ya 85: Mashabiki wa Yanga wanaongeza kasi ya kushangilia.

Dakika ya 80: Bao la tano kwa Yanga linapatikana kupitia kwa Emmanuel Martine ambaye anamalizia kazi ya Gadiel Michael.

GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO

Dakika ya 75: Chirwa anapambana kutengeneza nafasi lakini anashindwa kuwatoka walinzi wa Mbeya City.

Dakika ya 71: Juma Abdul wa Yanga yupo chini ameumia mguu.

Dakika ya 70: Mbeya City wanaonekana kupunguza kasi yao ya kujipanga.

Dakika ya 68: Mbeya City wanafanya mabadiliko, anatoka Mrisho Ngassa, anaingia Victor Hangaya.

Dakika ya 68: Yanga wanaendelea kulisakama lango la Mbeya City.

Chirwa anaipatia Yanga bao la nne akiunganisha pasi ya Ibrahim Ajibu.

GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO

Dakika ya 58: Kasi inaongezeka kwa Yanga wanaonekana kuwa wametulia zaidi.

Dakika ya 50 Obrey Chirwa anatupia kambani na kuandika bao la tatu

Dakika ya 50: GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO

Kikosi cha timu ya Mbeya City.

Dakika ya 47 Yanga wanapata penati

MAPUMZIKO

Dakika ya 45: Mwamuzi wa akiba anaonyesha dakika 4 za nyongeza, wakati huohuo, Martine wa Yanga yupo chini ameumia mguu wa kushoto.

Dakika ya 44: Ajibu anafika kwenye lango la Mbeya City lakini anakuwa ameotea.

Dakika ya 43: Buswita yupo chini ameumia, amechezewa faulo na Mwasapili ambaye amepewa kadi ya njano kwa mchezo mbaya.

Dakika ya 40: Kasi ya mchezo imepungua kiasi.

Dakika ya 34: Beki wa Yanga, Juma Abdul anapata nafasi ya kupiga sguti langoni mwa Yanga, mpira unatoka nje.

Dakika ya 32: Mbeya City wanapata faulo.

Dakika ya 30: Pius Buswita wa Yanga anabaki na kipa, miguu yake inapata kigugumizi, anashindwa kumalizia kazi nzuri aliyoifanya, mpira unaokolewa. Martine wa Yanga anapewa kadi kwa kucheza faulo.

Dakika ya 28: Mbeya City ni kama wameamka, wanajaribu kujipanga lakini mambo ni magumu.

Yanga wanafunga bao la pili kupitia kwa Emmanuel Martine, aliyewatoka walinzi wa Mbeya City na kufunga.

Dakika ya 22: GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO

Yanga wanapata bao la kwanza kupitia kwa Obrey Chirwa, anafunga baada ya uzembe wa mlinzi wa Mbeya City.

Dakika ya 19: GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO

Dakika ya 18: Mbeya City wanakuwa wabishi kuwaruhusu Yanga kucheza soka la pasi nyingi.

Dakika ya 14: Mbeya City wanalisogela lango la Yanga lakini wanakosa umakini.

Dakika ya 12: Mchezaji mmoja wa Mbeya City yupo chini akipatiwa matibabu.

Dakika ya 14: Mbeya City wanalisogela lango la Yanga lakini wanakosa umakini.

Dakika ya 12: Mchezaji mmoja wa Mbeya City yupo chini akipatiwa matibabu.

Dakika ya 6: Mchezo haina kasi kubwa.

Dakika ya 4: Kocha wa Yanga, George Lwandamina ameshasimama.

Dakika ya 1: Mchezo umeanza ka kasi ndogo.

Mwamuzi anaaznisha mchezo.

Huu ni mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom, unachezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

(LIVE UPDATES NA: NICOLAUS TRAC , GLOBAL PUBLISHERS)

Leave a Comment