×

Usajili Uwe Mikononi Mwa Makocha, Viongozi Kaeni Mbali

MTIBWA Sugar mnasta­hili pongezi kwa kuwa mmepam­bana mwanzo mwisho na ha­timaye kuweza kubeba taji la ushindi katika mashindano ya kombe la Uhai ambalo lili­husisha timu za vijana.

 

Mechi zenu zote kwenu zilikuwa fainali hata mechi ya mwisho ilikuwa ni fainali na mkafanikiwa kuibuka na ushindi. Mnastahili pongezi maana lile bao mlilolipata li­nastahili kuwekwa kwenye kumbukumbu.

 

Sasa ni wakati wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuta­zama upya namna ya kufanya maboresho kwa mashindano ya vijana kwa kuwa hii ya Uhai tayari imeshafanyika hivyo itakuwa vizuri kama kutakuwa na mbadala wake.

 

Kuongeza mashindano mengine pia ambayo yatawa­husu vijana yatafanya kuwe na chachu hasa kwa vijana kuwe­za kuimarika zaidi na kufanya timu zizidi kuwa na ushindani kwa kuwa muda mwingi zi­takuwa kwenye mashindano.

 

Hebu pata picha kwamba kwa sasa vijana hawatakuwa na mashindano mengine wa­takuwa huru wakisubiri tena michuano ya Uhai msimu ujao, kwa kweli hapa kuna vingi ambavyo shirikisho lina­wafanya vijana wakae bila kujishughulisha hili sio jambo jema hasa kwa kukuza vipaji vyao hivyo mashindano yawe mengi zaidi.

 

Tuachane na hayo turudi kwenye mada ya leo hasa ambayo nimeamua kuizun­gumzia, wakati wa maendeleo ya soka ni sasa ambapo timu nyingi zinakwenda kusajili wachezaji na nyingine zinak­wenda kuuza wachezaji.

 

Tayari vikumbo vimeshaan­za kupigwa, saini zinasainiwa na wengine wanaondoka ni jambo jema kwa kuwa tayari dirisha limefunguliwa hivyo ni wakati wa kila timu kuhak­ikisha kwamba i n a k a m i l i ­sha usajili ili kuboresha zai­di timu.

 

Hivyo, nap­enda kutoa rai sasa kwa vion­gozi wa timu kufanyia kazi mapendekezo ya mwalimu na sio kufanya kazi kwa ma­takwa yao bin­afsi ama kwa mapenzi yao ili waweze kusa­jili mchezaji kwenye timu.

 

Jambo hili la uongozi kuingil­ia mamlaka ya mwalimu sio la kufumbia macho hata kidogo kwa kuwa anayefundisha ni mwalimu ndiye anayejua ma­hitaji ya timu yake na upungu­fu wa kikosi chake ulipo.

 

Hivyo suala la kila kiongozi ama uongozi wa timu kumpangia aina ya wachezaji hali­leti afya kwa timu kwa kuwa kufanya hivyo kutasababi­sha mwalimu awe na kazi ngumu ka­tika kuhakikisha anakuwa na kikosi kizuri ambacho ki­tamsaidia kupata matokeo mazuri baadaye.

 

Timu inapopata matokeo mabaya uwanjani wa kwan­za kubeba mzigo wa lawama ni mwal­imu ambaye hakusikilizwa katika kufanya usajili sasa in­akuwaje apewe mzigo ambao huenda angeweza kuupungu­za wakati wa usajili kwa kusa­jili wachezaji ambao alikuwa na mahitaji nao?.

 

Jambo hili inabidi litiliwe mkazo na viongozi wote kwa kuhakikisha kwamba wana­fanya usajili kwa kutumia ripoti ya mwalimu ambayo imekabidhiwa hivyo kuna umuhimu wa kufanya mambo kwa sasa kitaalamu zaidi.

 

Viongozi wenye wachezaji wao mkononi wanapaswa wazingatie ripoti ya mwalimu ina taka kitu gani kwa kuwa hakuna timu ambayo itafan­ya usajili bila kupitia ripoti, litakuwa jambo la ajabu sana hasa kuelekea kwenye ligi am­bayo ina ushindani mkubwa sana.

 

Zama zimebadilika sana kwa sasa hivyo jambo la msingi ni mwalimu kusikilizwa map­endekezo yake ili kufanya kazi yake kwa uhuru hata itakapo­tokea amefanya vibaya aweze kujua namna ya kujipanga hasa kwa wachezaji ambao amewapendekeza hivyo ata­jua namna ya kuwatumia.