








LIKIWA na takribani miezi miwili mtaani, Gazeti la Betika limezidi kutikisa kila kona nchini ambapoleo Aprili 17 limemwaga masanduku (box) maalum kwa ajili ya wasomaji wa gazeti hilo kwa ajili ya kulipata bure kila linapotoka.
Gazeti hilo ambalo linachapishwa na Kampuni ya Global Publishers Ltd, hutolewa bure kwa watu wenye umri kuanzia miaka 18 kwenda juu.
Timu ya maofisa masoko wa Global Publishers imeingia mtaani leo Jumatano na kusambaza masanduku hay katika maeneo maalum kwa lengo la kuwarahisishia wasomaji wa Betika waweze kulipata kwa urahisi.
Akizungumza juu ya kusambaza ma-box hayo katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, Ofisa Masoko wa Global, Mussa Mgema, alisema:
“Kwa kuboresha zaidi katika Jiji la Dar es Salaam, tumesambaza maboksi maalum ambayo ndani yake kuna nakala nyingi za gazeti hilo ambapo msomaji anatakiwa kuchukua bure na kujipatia uhondo.
Betika lina kurasa 20 za rangi ambapo mbali na kuwa na makala na odds za kampuni mbalimbali, pia kuna takwimu za ligi kubwa barani Ulaya.