×

‘Shule ya Nape’ Yateketea kwa Moto Usiku

MABWENI ya Shule ya Sekondari Mtama, mkoani Lindi,  yameteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo ambapo  taarifa za awali zinasema hakuna majeruhi ila vitu vyote vilivyokuwa ndani vimeteketea.

Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye,  kupitia Twitter yake amesema wanafanya tathmini na uchunguzi wa chanzo cha tukio hilo.