
KUFUATIA wanafunzi wengi kukosa mikopo ya elimu ya juu na kudaiwa kuwepo figisu kwa wale wanaopaswa kupewa mikopo hiyo, Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (Daruso) imetoa saa 72 kwa Bodi ya Mikopo (HESLB) kutekeleza maagizo manne yafuatayo;
i. Ipeleke fedha za wanafunzi chuoni
ii. Irudishe fedha za wanafunzi zilizokatwa
iii. Iwapangie mikopo waliokata rufaa
iv. Imbadili Ofisa Mikopo chuoni hapo
