×

Mama Anayeishi Mazingira Magumu Alivyowezeshwa na Share Meal & Give Capital

Wanawake wanaounda kundi la Share Meal & Give Capital wakielekea kwa mwanamke huyo.

Hadija Said mkazi wa Kimara Kwa Mtoro Bonyokwa jijini Dar ambaye anayedaiwa kuishi katika mazingira magumu baada ya kifo mumewe na kuelemewa na familia, amesaidiwa mahitaji mbalimbali ikiwemo pesa ya mtaji na Wanawake wanaounda Kundi la Share Meal and Give Capital.

Mwenyekiti wa Kundi la Share Meal & Give Capital, Catherine Ambakisye maarufu Mama Rolaa (kulia) akimkabidhi sehemu ya msaada huo Bi. Hadija (anayepokea) wengine ni wanawake wanaounda kundi hilo.

Msafara wa Wanawake hao ukiongozwa na Mwenyekiti wao Catherine Ambakisye maarufu Mama Rolaa ulifika nyumbani kwa mwanamke huyo na kumpatia vitu mbalimbali ikiwemo vyakula, mafuta, sabuni na mahitaji mengine. Kinamama hao pia walimpatia kiasi fulani cha pesa kwa ajili ya kuanzisha biashara ndogondogo ya kujikimu.

Mjumbe wa eneo hilo Gaspar Ntokwa akimpongeza Mama Rolaa na wenzake baada ya kukabidhi msaada huo.

Baada ya kupewa msaada huo Bi. Hadija aliwashukuru wanawake hao na kuwaombea baraka kwa Mwenyezi Mungu na kuwaomba Wasamaria wema wengine kumsadia ili aweze kuishi na watoto watatu ambapo mmoja amefaulu kuingia kidato cha kwanza mwaka huu lakini amekumbana na kikwazo cha sare za shule madaftari na mengineyo.

Mnenguaji maarufu nchini, Queen Suzzy akimpa moyo wa ujasiri Bi Hadija na kumtaka akaze buti.

Mwanamke huyo ameomba kama kuna Wasamaria wema wengine wamsaidie kupitia namba yake ya simu ya mkononi 0658638684 jina la usajili Hadija Said.

Wakimpatia pesa ya kuanzia mtaji wa kujikimu.

Naye Mjumbe wa Shina wa eneo hilo Gaspar Ntokwa baada ya kushuhudia msaada huo ukitolewa aliwashukuru kinamama wanaounda kundi hilo na kuwaomba msaada wao usiishie hapo uwaangalie na wengineo kwa maana wenye shida kama hizo wape wengi sana na atawalipa kwa jinsi wanavyojitolea.

Kinamama hao wakiwa nyumbani hapo.

“Huyu mama ni mkazi wangu hapa mtaani namfahamu anavyoishi katika mazingira magumu tangu alipofiwa na mumewe na kumuachia watoto watatu hata hapa anapoishi kuna Msamaria mwema ndiye amemuhifadhi.

Bi. Hadija akitoa shukrani zake kwa Kundi la Kinamama Share Meal & Give Capital.

Hivyo msaada wenu una maana kubwa sana kwake na hata kwangu kama kiongozi wa eneo hili analoishi huyu mama”. Alimaliza kusema mjumbe huyo.

HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL

Leave a Comment