
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa msamaha kwa wafungwa 3, 826 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 58 ya muungano wa Tanzania.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumanne Aprili 26, 2022 na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni imeeleza kuwa msamaha huo unaenda sambamba na masharti mbalimbali ikiwa ni pamoja na wafungwa wote kupunguziwa robo ya vifungo vyao baada ya punguzo la kawaida la moja ya tatu linalotolewa chini ya kifungu cha 48(1) cha Sheria ya Magereza.
“Wafungwa hao sharti wawe wametumikia robo ya vifungo vyao na wawe wameingia gerezani kabla ya Februari 26, 2022 isipokuwa walioorodheshwa katika sharti la 2(1-11),” imeeleza taarifa hiyo.

