Rais Samia Apokea Kombe la Dunia (World Cup) Ikulu jijini Dar (Picha +Video)
Global Publishers May 31, 2022 0 Comments
SHARE THIS:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi pamoja na wadau mbalimbali wa michezo katika hafla ya kupokea Kombe la Dunia (World Cup) litakaloshindaniwa katika Mashindano ya Mpira wa miguu nchini Qatar, iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Mei, 2022.Rais Samia, akinyanyua juu Kombe la Dunia (World Cup) litakalo shindaniwa katika Mashindano ya Mpira wa miguu yatakayo fanyika nchini Qatar katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Mei, 2022.Rais Samia akipokea Kombe la Dunia kutoka kwa Balozi wa Kombe hilo kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Brazil Juliano.Rais Samia akipokea zawadi yenye mfano wa Kombe dogo la Dunia kutoka kwa Balozi wa Kombe hilo kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Brazil Juliano Belletti katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Mei, 2022.Rais Samia akiwa na Balozi wa Kombe la Dunia kutoka (FIFA) mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Brazil Juliano Belletti katika picha ya pamoja na wachezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’Wadau mbalimbali wa Michezo pamoja na Viongozi wakiwa kwenye hafla ya mapokezi ya Kombe la Dunia Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Mei, 2022.
RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo Mei 31, 2022, amepokea kombe la dunia, Ikulu jijini Dar es Salaam.