
KLABU ya Azam imemtambulisha kiungo mshambuliaji Abdul Seleman Sopu kama mchezaji wao mpya akitokea Coastal Union ya Tanga.

Sopu ambaye ndiye mfungaji bora wa michuano ya Azam Sports Federation Cup iliyomalizaka mwishoni mwa juma akiwa na magoli 9, akifanikiwa kuweka rekodi ya kufunga magoli matatu (Hat Trick) kwenye mchezo wa fainali ya michuano hiyo, waliyocheza dhidi ya Yanga
Amesaini mkataba wa miaka mitatu kuwatumikia wanalambalamba Azam Fc.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari ni kwamba mchezaji huyo alikuwa akihusishwa na vilabu vya Kariakoo vya Simba na Yanga lakini ni Azam FC ndiyo walioibuka kidedea kwa kuinasa saini ya kinda huyo ambaye alipita pia katika klabu ya Simba kabla ya kutimkia kwa Wanamangushi Coastal Union.