×

Rais Samia Ashiriki Mkutano Maalum Wa 20 Wa Wakuu Wa Nchi Jumuiya Ya Afrika Mashariki Nchini Burundi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza na Rais wa Rwanda Paul Kagame wakati wa Mkutano Maalum wa 20 wa Wakuu hao wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika Bujumbura nchini Burundi tarehe 04 Februari, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameshiriki Mkutano Maalum wa 20 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) tarehe 04 Februari, 2023

Rais Samia akiwa pamoja na Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki katika Mkutano Maalum wa 20 wa Wakuu hao wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais Samia akiwa amesimama pamoja na Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakati wa Wimbo wa Jumuiya hiyo ukipigwa kabla ya kuanza kwa Mkutano Maalum wa 20 wa Wakuu hao wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais Samia akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Bujumbura nchini Burundi.
Rais Samia akisalimiana na Rais wa Burundi, Évariste Ndayishimiye mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Bujumbura nchini Burundi.
Rais Samia akiwasili katika Ikulu ya Bujumbura nchini Burundi kwa ajili ya kushiriki Mkutano Maalum wa 20 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) tarehe 04 Februari, 2023.
Rais Samia akiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Melchior Ndadaye, Bujumbura nchini Burundi kwa ajili ya kushiriki Mkutano Maalum wa 20 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) tarehe 04 Februari, 2023

 

Leave a Comment