The House of Favourite Newspapers

Mbunge Shigongo Awapa Ujumbe Wanachuo ‘MUHAS’ ‘Usipuuze Kipaji Mungu Alichokupa”

0
Mbunge wa Jimbo la Buchosa Wilayani Sengerema, Mhe. Eric Shigongoo  na Mhamasishaji Maarufu Afrika Mashariki na Kati, ambaye pia ni Mjasiriamali na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Global Group akiwahutubia wanachuo Cha MUHAS namna ya kutumia vipaji walivyonavyo kuleta maendeleo.
Mbunge wa Jimbo la Buchosa Wilayani Sengerema, Mhe. Eric Shigongoo  na Mhamasishaji Maarufu Afrika Mashariki na Kati, ambaye pia ni Mjasiriamali na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Global Group,  amewataka  Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili. (MUHAS),
wanaosomea Udaktarii kutumia taaluma yao kutafuta mafanikio ya kimaendeleo.
Mhe Shigongo ameyasema hayo wakati akizungumza na wanachuo hao  jijini Dar es Salaam. Ambapo amewaeleza kuwa mbali na taaluma yao kwa kila mmoja kutumia ubunifu alionao katika kutengeneza fursa za kuleta maendeleo na kujikwamua.
Baadhi ya wanachuo wakifuatilia kwa makini hotuba ya Mhe. Eric Shigongo.
Samabamba na hayo Mhe Shigongo amegawa bure vitabu vyake mwenyewe.
Katika kuhitimisha hotuba yake, Mhe amefanya maombi ya pamoja maalumu katika kuwabariki wanachuo Kwa mafunzo wanayopata.
Ama Kwa hakika Kila Mmoja aliyekuwa amehidhuria amefurahia kuhamasishwa na mjasiliamali huyo.

Mhamasishaji huyo amewaeleza wanachuo hao kuwa kila binadamu ana nafasi yake ya kufanikiwa na kwamba  kinachotakiwa ni kujiamini na kuukataa mfumo unaowagandamiza hasa vijana na kuwanyima fursa ya kufanya maamuzi yao kwa uhuru.

“Naomba mnisikilize kwa makini, kijana uliyepo hapa leo na unayenisikiliza, una uwezo wa kufanya jambo kubwa na ukaacha alama siku ukiondoka duniani. Usisikilize watu wanachosema kuhusu wewe, ni Mungu tu aliyekuumba na kukupulizia uhai ndiye anafahamu makusudi ya kukuleta duniani na ukaacha alama hapa duniani.

“Amini kwamba unaweza kufanya jambo leo likabadili maisha yako na kukuondoa katika umasikini. Mimi familia yangu ilidharauliwa, niliitwa maskini, madaso na mjinga, nikaamini kwamba ni mjinga kweli, nikafeli darasa la saba na wala Sikwenda sekondari, lakini leo hii aliyeitwa mjinga ndiye ameshika hapa maiki. Ningeaamini maneno yao nisingekuwa Shigongo mnayeniona hapa,” alisisitiza.

Mwanafunzi kutoka kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Angel Frank akizungumza jambo.
Mwanafunzi kutoka kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Angel Frank akizungumza jambo kuhusiana na mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na baadhi ya wahamasishaji ambao ni wahitimu wa Chuo Cha MUHAS namna walivyotumia ubunifu wao kusaka mafanikio ikiwa njia mojawapo ya kuwatia moyo wanachuo wanaoendelea chuoni hapo.
Leave A Reply