

Msafara wa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, ukipokelewa katika eneo la Minjingu, Mkoa wa Arusha, Jumapili Juni 2, 2024, tayari kuanza ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo, baada ya kumaliza ziara katika Mkoa wa Manyara. Balozi Nchimbi ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Komredi Amos Gabriel Makalla na Katibu wa NEC, Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Komredi Rabia Hamid Abdalla.