×

Papa Francis Ataka Kusitishwa kwa Vita wakati wa Krisimasi

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis.

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis alishutumu mashambulizi ya kikatili ya shule na hospitali nchini Ukraine na Gaza katika sala yake  Jumapili kabla ya Krismasi.

“Wacha bunduki zinyamaze na nyimbo za Krismasi zisikie!” Papa Francis alisema wakati wa maombi yake jana siku ya Jumapili, ambayo aliitoa ndani ya kanisa hilo kama tahadhari kabla ya kipindi cha Krismasi chenye shughuli nyingi.

“Hebu tuombe kwamba Siku ya Krismasi kuwe na usitishaji wa mapigano katika nyanja zote za vita, nchini Ukraine, katika ardhi takatifu, Mashariki ya Kati na ulimwenguni kote,” Papa alisema.

Papa Francis alikumbuka, kama anavyofanya mara nyingi, mateso ya wanayopitia raia wa Ukraine, ambayo miji yake inaendelea kushambuliwa, “wakati fulani huharibu shule, hospitali na makanisa.”

Pia alisema alihisi uchungu alipofikiria kuhusu Gaza, “ukatili kama huo, bunduki zinazoua watoto, kulipua shule na hospitali.”

RAIS SAMIA ATEUA VIGOGO WAZITO KUTATUA MGOGORO wa NGORONGORO – YUMO MWALIMU wa SHULE NGORONGORO…

Leave a Comment