×

Simba Wapelekwa Arusha, Yanga Kutinga Mwanza Nusu Fainali ya Kombe la FA

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza rasmi viwanja vitakavyotumika kwa michezo ya Nusu Fainali ya michuano ya CRDB Federation Cup msimu wa 2025/26.

Mchezo wa kwanza utawakutanisha watani wa jadi Simba SC dhidi ya Coastal Union FC ambapo utapigwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Juni 20, 2026.

Kwa upande mwingine, mabingwa watetezi Young Africans S.C. maarufu Yanga watavaana na Azam FC katika mchezo mwingine wa nusu fainali utakaochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza Juni 21, 2026.

“KISU KILICHOTUMIKA KUKATA KICHWA cha TEMBA MKE wa MGANGA ALIKATIA VITUNGUU BILA KUJUA” – MSIMAMIZI

Leave a Comment