×

Mnyama Kunguruma Leo! Simba Kufanya Utambulisho wa Kikosi Kipya Uwanja wa Uhuru

Leo Agosti 8, 2026 ni siku kubwa kwa mashabiki wa Simba SC, huku klabu hiyo ikiandaa tamasha lake la Simba Day, ambalo litatumika rasmi kuwatambulisha wachezaji pamoja na benchi la ufundi kwa msimu wa 2026/2027 katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Simba Day imekuwa moja ya matukio muhimu kwa klabu hiyo, ambapo mashabiki hupata fursa ya kuiona timu yao mpya, wachezaji wapya pamoja na benchi la ufundi litakaloiongoza timu katika mashindano ya msimu mpya.

Katika tukio la mwaka huu, utambulisho wa kikosi na benchi la ufundi utahitimishwa kwa mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Kenya Police, mchezo unaotarajiwa kutoa picha ya awali kuhusu maandalizi ya Mnyama kuelekea msimu wa 2026/27.

Mchezo huo pia utakuwa fursa kwa benchi la ufundi kuwapima baadhi ya wachezaji na kuanza kujenga muunganiko wa kikosi kabla ya kuingia kwenye ratiba rasmi ya mashindano.

Kwa upande wa mashabiki, Simba Day inatarajiwa kuwa siku ya burudani na shangwe, huku macho mengi yakielekezwa kwenye sura mpya za kikosi hicho na namna ambavyo Simba itaanza safari yake katika msimu mpya.

Baada ya utambulisho huo, mchezo dhidi ya Kenya Police utakuwa sehemu ya kilele cha Simba Day, huku mashabiki wakisubiri kumuona Mnyama mpya wa msimu wa 2026/2027 akianza kuonyesha makali yake uwanjani.

Wachezaji 12 wa Kimataifa watakaotambulishwa na Simba Kuelekea Msimu Mpya 2026-27.

1:🇳🇪Mamadou T Kassali
2:🇨🇮Ismael Toure
3:🇿🇦Rushine De Reuck
4:🇸🇳Libase Gueye
5:🇨🇩Ellie Mpanzu
6:🇿🇦Neo Maema
7:🇿🇲Cloutas Chama
8:🇨🇮Anicet Oura
9:🇳🇬Ibraheem Jabaar
10:🇿🇦Keletso Makgalwa
11:🇲🇱Ibrahim Doumbia
12:🇨🇬Innocent Loemba

MAKAMU RAIS wa YANGA ARAFAT HAJI AWAPASUA SIMBA -“MWAKANI TENA -HATUJAOKOTAOKOTA WACHEZAJI KAMA WAO”

Leave a Comment