
JKT Tanzania imetoa ujumbe kupitia mitandao ya kijamii baada ya kukutana na Yanga SC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, huku ikionyesha heshima kwa ubora wa kikosi cha Wananchi na kuahidi kurejea ikiwa imara zaidi.
Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, JKT Tanzania iliandika:
“Uzuri kila mtu atakutana nao hawa jamaa, tutarudi tukiwa imara zaidi.”
Kauli hiyo imekuja baada ya JKT Tanzania kukutana na Yanga katika mchezo ambao Wananchi waliibuka na ushindi wa mabao 4-0.

Ujumbe huo unaonyesha namna JKT Tanzania inavyotambua ubora na ushindani wa Yanga, huku ikikiri kuwa kila timu inayokutana na mabingwa hao inapaswa kuwa tayari kwa changamoto kubwa.
Licha ya matokeo hayo, JKT Tanzania haijaonekana kukata tamaa, badala yake imeahidi kurejea ikiwa na nguvu zaidi katika michezo ijayo.

Kauli hiyo pia imeibua hisia na mijadala miongoni mwa mashabiki wa soka, huku wengi wakisubiri kuona kama JKT Tanzania itatimiza ahadi yake na kuonyesha kiwango bora katika michezo inayofuata.
Kwa Yanga, ushindi huo umeendelea kuipa mwanzo mzuri katika msimu mpya wa Ligi Kuu, huku JKT Tanzania ikitafuta namna ya kurekebisha makosa na kurejea katika ushindani.
Stori na Na Haika Urio | GPL -TUDACO